Msanii wa wiki

Msanii wa wiki
Msanii wa wiki - Aunt Ezekiel

Tangazo

Tangazo 2

Monday, February 17, 2014

Mjue Msanii wako - Bahati Bukuku









Bahati Bukuku ni mwanamuziki wa nyimbo za injili.




























Bahati Bukuku akiwa na Rose Muhando (katikati) na John Shabani (kulia)






Bahati Bukuku akiwa na msanii wa orijino Komedi Masanja mkandamizaji





Bahati Bukuku akiwa na muimbaji wa nyimbo za injili Rose Muhando




Bahati Bukuku akiwa na mwanamuziki mwenzake wa nyimbo za injili Boniface Mwaitege





Dunia Haina Huruma - Bahati Bukuku







Wewe ni Mungu - Bahati Bukuku







Waraka - Bahati Bukuku







Mapito - Bahati Bukuku






Lazima Usamehe - Bahati Bukuku





Mjue Msanii wako - Rose Ndauka








Rose Ndauka ni msanii, mwandishi, muongozaji wa Filamu Tanzania na pia ni mmiliki wa kampuni ya filamu ya Ndauka Entertainment. Rose Ndauka amezaliwa tarehe 7 mwezi wa 10 mwaka 1989 katika jiji la Dar es salaam. Rose alisoma mpaka form six katika shule ya Zanaki jijini Dar es salaam mwaka 2008.

Rose Ndauka alianza kuigiza rasmi mnamo mwaka 2007 kwenye filamU inayoitwa Swahiba ambapo aliigiza kama Aisha. Baada ya filamu hiyo Rose alipata nafasi ya kuigiza katika filamu mbalimbali kama vile Mahabuba, Solemba, Deception, Lost Adam n.k

Mwaka 2010 Rose Ndauka alifungua kampuni yake mwenyewe ya filamu inayoitwa Ndauka Entertainment, ambapo ameshatoa filamu mbili za Bad Girl na The Diary kupitia kampuni yake hiyo.

Rose Ndauka ana mchumba ambaye ni msanii wa Bongo flava aitwaye Malick Bandawe ambaye alikuwa anawakilisha kundi la TNG Squad kutoka Tanga. Rose na Malick Bandawe wamebarikiwa kupata mtoto mmoja anayeitwa Naveen Bandawe.












































Rose Ndauka akiwa na mchumba wake Malick Bandawe





Rose Ndauka akiwa na mchumba wake Malick Bandawe







Rose Ndauka akiwa na mchumba wake Malick Bandawe na mtoto wao Naveen Bandawe 






Rose Ndauka akiwa na mwanae Naveen Bandawe





Rose Ndauka akiwa na mwanae Naveen Bandawe





Mjue Msanii wako - Emmanuel Mgaya a.k.a Masanja Mkandamizaji








Emmanuel Mgaya maarufu kwa jina la Masanja Mkandamizaji ni mchekeshaji maarufu na muimbaji wa muziki wa injili nchini.

































Masanja Mkandamizaji akiwa na msanii Shilole walivyotembelea Washington DC nchini Marekani







Nyumba yake





Mjue Msanii wako - Joti






Lucas Lazaro Mhuvile ambaye anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii la Joti, ni muigizaji wa kundi la Orijino Komedi lililokua likijulikana kama Ze Comedy zamani ambapo michezo yake huonyeshwa kwenye televisheni ya TBC1. 

Joti amezaliwa tarehe 9 Julai mwaka 1982, katika mkoa wa Morogoro wilaya ya Ulanga katika kijiji cha Biro.

Joti ni msanii mwenye kipaji kikubwa sana, kwani ana uwezo wa kucheza kama mwanamke, mzee kikongwe, mtoto n.k.

Joti alipitia vikundi kadhaa vya maigizo kabla ya kujiunga na kundi lake la Ze Comedy zamani na sasa orijino Komedi analofanyia kazi kwasasa. Mwaka 2000 mpaka 2001 Joti alikuwa mwigizaji katika kundi la Nyepenyo, baadaye mwaka 2001 mpaka 2002 alijiunga na kundi lingine la Sun Rise na mwaka 2002 mpaka 2003 alikuwepo kwenye kundi la Nyota Ensemble.

Joti pia anajulikana kwa majina mengine kama Hami Jay, Da Kiboga, Mzee Simbawanga, Asha Ngedere, Andunje na Joti Mdebwedo.










Joti akiwa na msanii Sandra







Joti akiwa na mtangazaji wa Clouds FM Zamaradi Mketema







Joti akiwa na mtangazaji wa Clouds FM Zamaradi Mketema







Joti akiwa na wasanii wenzake wa Orijino Komedi, kutoka kushoto ni: Joti, Wakuvanga, Mpoki, Masanja Mkandamizaji, na Mac-Regan







Joti akiwa kwenye shughuli zake za usanii


















Mjue Msanii Wako - Zuwena Mohamed a.k.a Shilole









Zuwena Mohamed ambaye ni maarufu sana kwa jina lake la uigizaji Shilole ni muigizaji wa Bongo movies na ni msanii wa muziki wa mduara. Shilole ni mama wa watoto wawili. Kwasasa Shilole anatamba sana na vibao vyake kama Nakomaa na Jiji, Paka la Baa n.k.



















































Shilole akiwa na Masanja Mkandamizaji walivyokuwa Marekani






Saturday, February 1, 2014

Mjue Msanii Wako - Ndumbangwe Misayo "Thea"








Ndumbangwe Misayo ambaye anajulikana sana kwa jina la uigizaji la Thea, ni mtoto wa kwanza katika familia ya Matilda Misayo na Gaudence Urassa. Thea alizaliwa mwaka 1982 mkoani Shinyanga kabla ya kuhamia Dar es salaam na wazazi wake, ambako alipata elimu ya msingi katika shule ya Mapambano, Sinza, na baadaye kujiunga na sekondari ya Zanaki, alikosoma hadi kidato cha Tatu kabla ya kuhamia Greens Victoria, alikohitimu kidato cha nne mwaka 2001.

Thea alijiunga na kikundi cha Mambo Hayo akiwa kidato cha kwanza tu, hata hivyo baada ya kundi la Mambo hayo kusambaratika Thea alihamia Kaole.

Baadhi ya filamu alizocheza hadi sasa ni Dadaz, Ukungu, Dunia Yangu, Revenge, Sigito, Tone la Damu, Why Me, Solemba, Born to Suffer, Simanzi ya Moyo, Trip to America, Out of Love na Bed Rest.

Thea ni mshindi wa tuzo ya vinara mwaka 2008 kama mwigizaji bora wa kike pia ni mama wa mtoto mmoja wa kiume.





Ndumbangwe Misayo a.k.a Thea akiwa na mume wake Mike Sangu siku ya harusi yao