Msanii wa wiki

Msanii wa wiki
Msanii wa wiki - Aunt Ezekiel

Tangazo

Tangazo 2

Monday, March 24, 2014

Mjue Msanii Wako - Marlaw














Msanii Marlow akiwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete






Marlaw (kushoto) akiwa na msanii mwenzake wa Bongo Fleva Nasib Abdul a.k.a Diamond Platnumz





Mjue Msanii Wako - Professor Jay








Professor Jay ambaye jina lake halisi ni Joseph Haule ni mwanamuziki wa Bongo Fleva ambaye anaimba sana nyimbo za Hip Hop.

Professor Jay alizaliwa tarehe 29 mwezi wa 12 mwaka 1975.

Professor Jay alianza muziki mwaka 1994 akiwa mmoja wa memba kwenye kundi la Hard Blasters ambalo lilikuwa likijulikana sana na kibao chao cha Chemsha Bongo, wakati huo Professor Jay akitumia jina la Nigga J.

Alianza kuimba mwenyewe akiwa msanii anayejitegemea mwaka 2001, na ametoa nyimbo nyingi kali kama vile Nikusaidieje, Zali la Mentali, Piga Makofi, Ndio Mzee, Ndivyo Sivyo n.k















Mjue Msanii Wako - Juma Nature







Juma Nature ambaye pia anajulikana kama Sir Nature ni msanii wa Bongo fleva ambaye anaimba sana nyimbo za hip hop. 

Juma Nature ambaye jina lake halisi ni Juma Kassim Kiroboto alizaliwa mwaka 1980. 

Juma Nature ndiye alikuwa ni muanzilishi wa kundi la muziki lililokuwa likijulikana sana la Wanaume Family na maskani yake yakiwa Temeke jijini Dar es salaam.

Mwezi wa 11 mwaka 2006 kundi la Wanaume Family liligawanyika na Juma Nature alijitoa kutoka kwenye kundi hilo akiwa na baadhi ya wasanii wachache kutoka kwenye kundi hilo la Wanaume Family na kuanzisha kundi lingine la Wanaume Halisi ambalo linavuma mpaka sasa.












Juma Nature na mke wake Pili, siku ya harusi yao







Juma Nature na Lady Jaydee








Juma Nature (kushoto) akiwa na msanii mwenzake Mh. Temba (kulia)