Msanii wa wiki

Msanii wa wiki
Msanii wa wiki - Aunt Ezekiel

Tangazo

Tangazo 2

Monday, February 17, 2014

Mjue Msanii wako - Rose Ndauka








Rose Ndauka ni msanii, mwandishi, muongozaji wa Filamu Tanzania na pia ni mmiliki wa kampuni ya filamu ya Ndauka Entertainment. Rose Ndauka amezaliwa tarehe 7 mwezi wa 10 mwaka 1989 katika jiji la Dar es salaam. Rose alisoma mpaka form six katika shule ya Zanaki jijini Dar es salaam mwaka 2008.

Rose Ndauka alianza kuigiza rasmi mnamo mwaka 2007 kwenye filamU inayoitwa Swahiba ambapo aliigiza kama Aisha. Baada ya filamu hiyo Rose alipata nafasi ya kuigiza katika filamu mbalimbali kama vile Mahabuba, Solemba, Deception, Lost Adam n.k

Mwaka 2010 Rose Ndauka alifungua kampuni yake mwenyewe ya filamu inayoitwa Ndauka Entertainment, ambapo ameshatoa filamu mbili za Bad Girl na The Diary kupitia kampuni yake hiyo.

Rose Ndauka ana mchumba ambaye ni msanii wa Bongo flava aitwaye Malick Bandawe ambaye alikuwa anawakilisha kundi la TNG Squad kutoka Tanga. Rose na Malick Bandawe wamebarikiwa kupata mtoto mmoja anayeitwa Naveen Bandawe.












































Rose Ndauka akiwa na mchumba wake Malick Bandawe





Rose Ndauka akiwa na mchumba wake Malick Bandawe







Rose Ndauka akiwa na mchumba wake Malick Bandawe na mtoto wao Naveen Bandawe 






Rose Ndauka akiwa na mwanae Naveen Bandawe





Rose Ndauka akiwa na mwanae Naveen Bandawe





No comments:

Post a Comment