Msanii wa wiki

Msanii wa wiki
Msanii wa wiki - Aunt Ezekiel

Tangazo

Tangazo 2

Wednesday, July 3, 2013

Msanii wa Ze Comedy Masanja Mkandamizaji na Shilole Watua Washington DC Marekani




Wasanii Masanja Mkandamizaji na Shilole wakiwa Washington DC  nchini Marekani, walikokwenda kwa ajili ya kutumbuiza kwenye sherehe ya miaka 3 ya vijimambo na tamasha la utamaduni wa kiswahili.


Masanja na Shilole wakiwa nje ya jengo la ubalozi wa Tanzania Washington DC nchini Marekani, Jumapili June 30, 2013


Masanja Mkandamizaji na Shilole wakiwa na Asha Riz mjumbe aliyewawakilisha Tano Ladies kuwapokea wasanii hao mara tu walipowasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dulles uliopo Sterling Virginia.


Shilole


Shilole na Masanja Mkandamizaji wakiwa na mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya sherehe ya miaka 3 ya vijimambo Bwana Baraka Daudi mara baada ya kuwapokea.


Shilole na Masanja wakiwa na kaimu Balozi wa Tanzania nchini Marekani mama Lily Munanka (katikati) pamoja na mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya sherehe ya miaka 3 ya vijimambo na tamasha la utamaduni wa kiswahili Marekani Bwana Baraka Daudi (kushoto) na Rais wa jumuiya ya watanzania DMV (kulia) Bwana Iddi Sandaly walipotembelea ubalozi wa Tanzania nchini Marekani uliopo Washington DC.


Masanja na Shilole wakifanya shopping 

No comments:

Post a Comment